Amos 1:6-10

6 aHili ndilo asemalo Bwana:

“Kwa dhambi tatu za Gaza,
hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.
Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima
na kuwauza kwa Edomu,
7 bnitatuma moto juu ya kuta za Gaza
ambao utateketeza ngome zake.
8 cNitamwangamiza mfalme wa Ashdodi
na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni.
Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni,
hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,”
asema Bwana Mwenyezi.
9 dHili ndilo asemalo Bwana:

“Kwa dhambi tatu za Tiro,
hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu.
Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu,
na kutokujali mapatano ya undugu,
10 eNitatuma moto kwenye kuta za Tiro
ambao utateketeza ngome zake.”
Copyright information for SwhNEN